|
Update Kuhusu Kitengo cha Misiba |
|
|
|
|
Sunday, 06 September 2009 |
Assalaam Alaykum.Kutokana na kumbukumbuku zetu inaonesha bado ada za kuchangia mfuko wa Misiba hazitolewi kwa wakati na baadhi yetu tumejisahau kabisa.Kuna wachangiaji ambao wana malimbilikizo kutokea 2007 na kwa maana hii ni kuwa hata 2009 bado hali ya uchangiaji si ya kuridhisha hata kidogo.Tulikuwa na utaratibu wa kuandikiana kwa madhumuni kukumbushana kila baada ya muda kuhusu uchangiaji lakini kwa bahati mbaya haukufanya kazi na baadae kitengo kikaamuwa kuondoa ule utaratibu wa kumfuta mchangiaji mwenye malimbikizo lakini pia matunda yake sio ya kuridhisha.Kupunguwa kwa gharama za mazishi kutokana na mabadiliko ya mfumo wa mazishi yetu ( kuzika bila ya kupitia kwa Mkurugenzi wa Mazishi), kitengo cha Misiba kinafikiria kutowa ubani kwa wachangiaji ambao wana familia zao nyumbani ikiwa ni baba na mama mzazi, mke na mtoto wa kumzaa.Kiwango kitaamuliwa baada ya kupitishwa na ngazi zote za Jumuiya.Watakaofaidika na ubani huu ni wale ambao watakaokuwa wamelipia ada zao bila ya kuwa na malimbikizo yasiyozidi miezi mitatu.Kama ni miongoni mwa walio na malimbikizo jitahidi kulipa mapema na tunakushauri kutumia njia ya Standing order ambayo itakusaidia sana kuondokana na usumbufu huu.Kitengo kinawatakia Ramadhaan njema na Insha Allah Moja atukubalie funga zetu na ibada zetu zote katika mwezi huu na iwe ni Darsa kwa miezi yote katika maisha yetu Amin.Wabillah Tawfiyq.
|
|
Last Updated ( Friday, 16 October 2009 )
|